MH. KOKA KUTEMBELEA MAMBO SAFI GROUP

“MAMBO SAFI GROUP” tarehe 06/01/2013 tutatembelewa na Mh. Koka mbunge wa jimbo la kibaha mjini atakaeambatana na mama Serina Koka na viongozi wengine wapatao watano kimara Baruti Dar Es Salaam. “MAMBO SAFI GROUP” tupo katika maandalizi ya kupokea viongozi wa ngazi ya kitaifa na kata ya Kimara hapo tarehe 31/01/2013, lengo ni kuona shughuli zinazo tekelezwa na MAMBO SAFI GROUP. Pia kuongea na vijana na akina mama wapatao mia nne (400) katika masuala ya maendeleo ya ujasiliamali, michezo na sanaa. Mafunzo enedelevu ya ujasiliamali, Jinsia, Michezo, Sanaa na Afya, utalii na Afya, Tamaduni na kuanzisha mkakati ambao utalete tija katika jamii. Mratibu wa Ukimwi manispaa ya Kinondoni ameitimisha mafunzo ya kwanza ya Ujasiliamali kwa akina mama Wajane wanaoishi na Virusi vya Ukimwi, hii ni kutokana na mafunzo endelevu yanayotolewa na “MAMBO SAFI GROUP”

0 comments
 
Mambo Safi Group © 2014 | JM Designs